For faster navigation, this Iframe is preloading the Wikiwand page for Natal.

Natal

Ramani inaonyesha eneo la jimbo la Natal (na. 4, rangi nyekundu-nyeupe) pamoja na maeneo ya KwaZulu (njano) ndani ya Afrika Kusini kabla ya 1994

Natal ilikuwa koloni ya Uingereza katika Afrika ya Kuini-Mashariki tangu 1856. 1910 ikaingia kama jimbo la Natal katika Muungano wa Afrika Kusini pamoja na koloni nyingine za Rasi, Transvaal na Dola Huru.

1994 jimbo la Natal liliunganishwa na bantustan ya KwaZulu kuwa jimbo jipya la KwaZulu-Natal.

Historia ya awali

[hariri | hariri chanzo]

Jina la Natal limetokana na mpelelezi na mbaharia Mreno Vasco da Gama aliyefika kwenye pwani karibu na Durban mnamo 25 Desemba 1497. Aliita mahali Rio de Natal au "mto wa Krismasi" kutokana na tarehe ya kufika kwake. Jina limebaki kwenye ramani likaendelea kutumiwa kwa eneo hili.

Mwaka 1824 mfalme Shaka Zulu alikutana hapa na kikosi cha Waingereza akawa rafiki wa afisa kiongozi akampa zawadi ya kanda la eneo lenye urefu wa maili 25 kwenye pwani na upana wa maili 100 kuingia barani. Waingereza hawakujaribu kutawala eneo hili lote lakini walianzisha makazi ya Port Natal yaliyokuwa baadaye mji wa Durban.

1839 kundi la makaburu aina ya voortrekker lilifika Natal na kuanzisha mji wa Pietermaritzburg iliyokuwa mji mkuu wa jamhuri ndogo ya Natalia.

Baada ya miaka mitatu Waingereza kutoka rasi 1842 walitwaa jamhuri ya makaburu kwa nguvu ya kijeshi na kuiunganisha na koloni ya rasi. Makaburu wengi waliondoka kwenda eneo ng'ambo ya mto Oranje walipoanzisha Dola Huru ya Oranje.

Natal ilitawaliwa kwa muda kama sehemu ya rasi lakini ikapewa cheo cha koloni ya pekee kuanzia 1856.

Natal ni eneo la Zulu hasa. Kuna kundi kubwa ya watu wenye asili ya Uhindi waliopelekwa hapa na Waingereza kama wafanyakazi kwenye mashamba ya miwa na katika migodi wakati wa karne ya 19. Makaburu walibaki wachache tu na Watu wenye asili ya Kiingereza waliingia hapa kutoka rasi.

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Natal kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
{{bottomLinkPreText}} {{bottomLinkText}}
Natal
Listen to this article

This browser is not supported by Wikiwand :(
Wikiwand requires a browser with modern capabilities in order to provide you with the best reading experience.
Please download and use one of the following browsers:

This article was just edited, click to reload
This article has been deleted on Wikipedia (Why?)

Back to homepage

Please click Add in the dialog above
Please click Allow in the top-left corner,
then click Install Now in the dialog
Please click Open in the download dialog,
then click Install
Please click the "Downloads" icon in the Safari toolbar, open the first download in the list,
then click Install
{{::$root.activation.text}}

Install Wikiwand

Install on Chrome Install on Firefox
Don't forget to rate us

Tell your friends about Wikiwand!

Gmail Facebook Twitter Link

Enjoying Wikiwand?

Tell your friends and spread the love:
Share on Gmail Share on Facebook Share on Twitter Share on Buffer

Our magic isn't perfect

You can help our automatic cover photo selection by reporting an unsuitable photo.

This photo is visually disturbing This photo is not a good choice

Thank you for helping!


Your input will affect cover photo selection, along with input from other users.

X

Get ready for Wikiwand 2.0 🎉! the new version arrives on September 1st! Don't want to wait?